Mashariki ya Kati

Article on other languages:

del.icio.us del.icio.us
Digg Digg
Furl Furl
Reddit Reddit
Rojo Rojo
Add to OnlyWire
Mashariki ya Kati pamoja na Uturuki

Mashariki ya Kati ni namna ya kutaja sehemu kubwa ya Asia ya Magharibi.

Kwa kawaida nchi zifuatazo huhesabiwa humo:

Nchi hizi zinatajwa pamoja kwa sababu zina historia ya pamoja na utamaduni ni wa karibu kati yao.

Matatizo ya jina hili

Jina la "Mashariki ya Kati" limesambazwa kutokana na kawaida ya Kiingereza na kutafsiriwa katika lugha mbalimbali. Lina matatizo kadhaa yanayotakiwa kujulikana hata tukiendelea kutumia jina:

  • kuna namna mbalimbali za kutaja nchi za zaida zinazohesabiwa humo au la (kwa mfano: wengine huhesabu pia nchi za Asia ya Kati kama vile Kazakhstan, Kyrgyzstan, Tajikistan n.k.)
  • jina ni tamko la Kiulaya: nchi hizi ziko upande wa mashariki kwa mtu aliyeko Ulaya. Kutoka Uswahilini ingekuwa zaidi "Kaskazini ya Kati"
  • matumizi ya jina yamebadilika: zamani Kiingereza kilitofautisha kati ya
    • "Mashariki ya Karibu",
    • "Mashariki ya Kati" na
    • "Mashariki ya Mbali"

kikimaanisha

Lugha mbalimbali za Ulaya Bara kama Kijerumani zinaendelea kutumia majina haya matatu vile. Pia wataalamu wa historia kwa Kiingereza hupendelea kutofautisha kati ya "Mashariki ya Karibu" na "Mashariki ya Kati".



Image:WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Mashariki ya Kati" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Mashariki ya Kati kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.

This article is from Wikipedia. All text is available under the terms of the GNU Free Documentation License.