|
Article on other languages:
|
Fedha (kisayansi pia: ajenti/agenti kutoka Kilatini "argentum") ni elementi na metali yenye kifupi cha Ag na namba atomia 47 katika mfumo radidia. Uzani atomia ni 107.86. Ajenti huyeyuka kwa 1234,93 K (961,78 °C) na kuchemka kwa 2435 K (2162 °C). Kiasili yatokea kama metali nyeupenyeupe na laini au kama mchanganyiko katika madini. Kati ya metali zote fedha ni wayaikaji na inapitisha vizuri umeme. Fedha - PesaHuhesabiwa kati ya metali adimu na katika historia imetumiwa mara nyingi kama metali ya sarafu. Mara nyingi kwa Kiswahili neno "fedha" latumiwa sawa na "pesa" au "sarafu". |
This article is from Wikipedia. All text is available under the terms of the GNU Free Documentation License.